Sunday, March 10, 2013

WALIONIFUNGAWALIISHIA KUPIGWA

Na Mch. Maximillian Machumu




                                     Mchungaji Maximillian Machumu (RP) akihubiri  jumapili hii



Waamuzi 15:9-16: Samson alikuwa mnadhiri wa Mungu na aliwekwa kuwaangamiza wafilisti, kwasababu ya kuwaangamiza Wafilisti ndugu zake wakaamua kumfunga na kumkabidhi kwa wafilisti ili wasije kulipa kisasi kwa wao. Katika kumfunga Samsoni, ndugu zake wapatao elfu tatu walitumia kamba mbili; kuna mambo mengi ya kujifunza kupitia habari hii ya Samsoni:



KWANINI NDUGU WALIMFUNGA: kama tulivyosoma katika kitabu cha Waamuzi 15:9-16, ndugu zake ndio waliohusika kumfunga Samsoni. Hapa tunajifunza kuwa mara nyingi adui (shetani) anapotaka kumfunga mtu hupitia kwa watu wake au wanaomjua mtu huyo vizuri. Kifungo kinachotokana na watu wako wa karibu ni kibaya zaidi kwasababu wanaujua udhaifu wako; muda gani unaomba na muda gani huombi.

Ndio maana hata Mtume Paulo aliwahi kutegeshewa nyoka kwenye kuni (Matendo ya Mitume 28:3). Nyoka ni yule mtu wa karibu anayejua siri na mambo unayoyafanya, kwasababu hiyo inakuwa rahisi kwa shetani kuwatumia kukuangamiza. Nyoka hakuonekana mwanzoni kwa Paulo kwasababu alijifanya kama kuni, na watu wa karibu ni vivyohivyo huwezi kuwatambua kwa urahisi. Furaha ni kuwa Mungu hakuruhusu yule nyoka kumwangamiza Mtume Paulo.



KWANINI WALITUMIA KAMBA MBILI: Ndugu wa Samsoni walikuwa elfu tatu lakini jambo la ajabu ni kuwa walibeba kamba mbili tu; Utajiuliza nini siri ya hizi kamba mbili?. Yesu mwenyewe aliainisha kamba mbili kuu ambazo shetani anazitumia kuwaangamiza na kuwafunga watu duniani. Ukisoma katika Ufunuo 1:18 “na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.” Kumbe zile kamba mbili zina maana ya mauti na kuzimu. Kuzimu inaleta magonjwa na matatizo mbalimbali lakini mauti inaleta kifo. Kamba mbili mpya ni mauti na kuzimu. Kwa kuzimu na mauti shetani amekuwa akiwaangamiza na kuwatesa watu wa Mungu. Inawezekana na wewe ni mmoja wa watu wanaoteseka kwasababu ya kamba hizi leo kuna habari njema kuwa Yesu aweza kukata kamba hizo.



MATOKEO YA KIFUNGO CHA SAMSONI: baada ya kumfunga, ndugu zake wakamkabidhisha kwa wafilisti yaani adui zake. Jambo la ajabu likatokea, mara baada ya kukabidhiwa. Imeandikwa, “Alipofika Lehi, Wafilisti wakapiga kelele walipokutana naye; ndipo roho ya Bwana ikamjia kwa nguvu, na zile kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitani iliyoteketezwa kwa moto, na vile vifungo vyake vikaanguka mikononi mwake.” Waamuzi 15:14 kupitia kifungo kile Mungu akamtumia Samsoni kuwaangamiza wafilisti wote. Kumbe waweza upo katika kifungo ambacho Mungu alikiruhusu ili upate ushindi ulio mkamilifu.



MUNGU ANAWEZA KUKATA KAMBA ZILIZO KATIKA MAISHA YAKO: Wachawi na waganga wanaweza kuwa wajanja mbele ya macho yetu lakini Bwana anawaona, na kamba zao zinaonekana mbele ya macho ya BWANA. Hata mfalme Daudi aliwahi kuwa katika kamba hizo ukisoma katika Zaburi 119:61 “Kamba za wasio haki zimenifunga, Sikuisahau sheria yako.” Upo uwezekano wa mtu kufungwa, Mwilini unajiona ni mtu asiye na mafanikio au asiye na mwelekeo lakini rohoni unakuwa umefungwa na kamba kabisa. Zaburi 18:1->… “…Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu. Kamba za kuzimu zilinizunguka, Mitego ya mauti ikanikabili. Katika shida yangu nalimwita Bwana, Na kumlalamikia Mungu wangu. Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake, Kilio changu kikaingia masikioni mwake…” Mungu anaweza kukutoa katika kamba za matatizo unayopitia. Daudi alipokuwa katika kamba hizo aliliitia jina la BWANA.



Yesu alipofufuka akatangaza kuwa anazo funguo za mauti na kuzimu, Hata kama aliyekufunga awe mtu wa karibu kiasi gani lakini zipo funguo za kufungua kamba zilizokufunga. Kama alivyofanya kwa Samsoni; baada ya kukufungua kinachofuata ni kipigo kwa wale wote walioshiriki kukufunga. Mungu anaweza kukutofautisha; shida na mateso yote unayopitia si kitu mbele za Mungu wetu kwasababu yeye anaweza kukuweka huru. Mpokee Yesu upate uhuru mkamilifu, kwasababu dunia ya leo haipo salama kama haupo ndani ya Yesu.

Saturday, March 9, 2013

FAHAMU NINI MAANA YA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA







Nini maana ya kusifu na kuabudu
KUSIFU NA KUABUDU ni maneno
tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu
MAANA --- nikuelezea wasifu au
wajihi za kitu au mtu. Sasa
tunaposema tunamsifu Mungu
inamaanisha ni KWA KUMUINUA
JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA
SAUTI,KUFANYIA SWANGWE,
KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA
UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4
Neno hili kusifu kwa kiebrania
lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa
kuongeza vionjo na mbwembwe
zaidi. Mfano neno haleluya
unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee)
Tehila ni kuwa kama kichaa
unaposifu au kuabudu kwa utukufu
wa Bwana. (Nilidhani labda hapa
ndipo waswahili walipopata neno
taahila).
Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu
(you just surrender yourself to the
Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za
Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni
yeye peke yake anayestahili heshima
na utukufu. Huwezi kumpigia saluti
mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia
ya kumwabudu Mungu katika roho
na kweli ndipo tunapomwona kama
alivyo na utukufu wake
2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina
maana ya kuabudu, kusujudia,
kuinama kwa kuonesha
unyenyekevu, kuonesha heshima
kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno
la Agano la Kale proskuneo
halikadhalika lina maana ya kubusu
mkono, au kupiga magoti na kugusa
ardhi kwa paji la uso kwa
unyenyekevu mkuu. Maneno
mengine mawili ya kuabudu yana
maana ya kutumika, kufanya ibada
Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.
Waache Watu Wangu Waondoke, Ili
Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu
alilolirudia mara kwa mara lilipelekea
Farao kuwaruhusu watu wa Mungu
kutoka Misri. Tangu wakati huo,
Mungu, Mungu mwenye wivu,
amekuwa akipambana na watu wake
akiwazuilia kuabudu miungu mingine
na sanamu, na badala yake
wamwabudu Mungu aliye hai na wa
kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na
kumfurahia daima. Mungu
anawatafuta watu wa kumwabudu,
na kufanya ibada ndiyo wito wetu
wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja,
tena ipo, ambapo wale waabuduo
halisi, watamwabudu Baba katika
roho na kweli. Watu wanaoabudu
namna hii, ndio Baba anawatafuta.
Msitari wa 24 unasema Mungu ni
Roho na wote wanaomwabudu
imewapasa kumwabudu katika roho
na kweli.). Ibada ya kweli ni pale
tunapomruhusu Roho Mtakatifu
atuongoze kutoka katika roho zetu
au mioyo yetu kuabudu katika roho
na katika kweli na sio tumaini letu
ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.
Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni
la kipekee na linamhusu Mungu
(utatu mtakatifu) ambao peke yao
wanastahili. Lucifer, aliyekuwa
mhusika mkuu wa ibada huko
mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa
ajili yake, maana yake aabudiwe
yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo
lililopelekea kuanguka kwake (Isaya
14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani
alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe
falme zote za dunia lakini Bwana
alikataa Mt4:8-10.
Kwa hiyo kuabudu ni ibada na
tunaposema ibada sio zile taratibu
za kibinadamu tulizojipangia katika
ibada zetu za siku za leo, ibada za
leo tumeweka mambo mengi sana
na yanatumia muda mwingi sana
kuliko ile maana hasa ambayo
mungu aliikusudia katika agano la
kale utana ibada zilikuwa zinafaywa
kwa mambo makuu 2 neno la
Mungu, na Kuabudu.
Kuabudu ni sehemu ya maisha
wanadamu tumeumbiwa kuabudu,
watuwezi kuishi bila kuabudu hapa
haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza
kuwa unaabudu Mungu wa kweli au
miungu kama ambavyo ukisoma bilia
utaona kuna miungu mingi inatajwa
mfano Baali, Dagon ink na hata leo
iko miungu mingi ambayo wanadamu
wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni
mmoja tu. Na katika biblia tunaona
kuaudu kwa mara ya kwanza
kulikofanywa na Ibrahimu kutoka
katika kitabu cha mwanzo 12: 8
Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa
kumwabudu Mungu kila wakati.
Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu
kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm
29:2 Tunapomwabudu mungu naye
Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah
3:17 Rom 12:1-2
Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano
wa mungu ulivyo ndani yako,
haijarishi unaabudu wapi uwe peke
yako au mko wengi kama unaabudu
kwa kutokumaanisha au kumaanisha
itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu
anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo
wako kwa Mungu wako.
KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA
KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26
zinaonyesha ambavyo kwa kutumia
kusifu tu Mungu alishuka na kufanya
lile lililokuwa hitaji lao.
Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa
unasifu na kuabudu humfukuza adui
mbali kutokana na ukiwa kwenye
ibada Mungu hushuka maana yeye
anasema anakaa katikati ya sifa
hivyo palipo na Mungu shetani
hawezi kuwepo lazima akae
mbali.akimbie mbali kabisa maana
kunakuwepo na uwepo wa bwana
wa Majeshi.
Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu
Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa
Zaburi ya 100 inatuelekeza namna
ya kuanza, lakini zaidi ya yote
tunapaswa kuishi maisha ya ibada
bila kukoma. Kwa kila tunapopumua,
kwa kila wazo, kwa neno na tendo,
tunapaswa kumwabudu Mungu wetu
mzuri tunayemtumikia milele na
milele Zab 145:1,2
mwa 12:6- Siku zilipita na watu
wakafanyia ibada kwenye Hekalu na
kwenye masinagogi; lakini siku hizi
miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor
6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada
zinatakiwa zifanyike kila wakati na si
mara moja kwa wiki kama wengine
wanavyo dhani.
Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu
walivyotumia mioyo yao, mawazo
yao, mikono yao, viganja vyao, miguu
yao, na midomo yao katika uimbaji.
Walipaza sauti zao kwa furaha na
kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki
na kushukuru.
Maneno kama halal na haleluya
kutoka katika Zaburi yana maana ya
kusifu, kumwinua na
kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah
lina maana ya kunyoosha mikono
hewani, na neno barak lina maana ya
kupiga magoti katika ibada ya
kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu
katika kumhudumia Mungu na
mwanadamu ni ibada pia (Rum
12:1). Watu pia humwabudu Mungu
katika sanaa zao, katika uandishi
wao, katika michezo ya kuigiza,
katika muziki, katika usanifu wa
majengo, na hata katika utoaji wa
fedha zao kwa ajili ya Injili.
Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na
kuabudu ni kuimba tu hapana kuna
njia nyingi za kusifu au kuabudu,
unaweza kutumia sanaa nyingine
kumwabudu mungu au watu
wengine wakamwabudu Mungu mf
maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji,
upambaji au unakshi wa vitu,
kujenga .nk
Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu
yanapaswa kujawa na zaburi,
nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo
zinaweza kuongozwa na Roho katika
lugha mpya anazotupatia Yeye.
Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa
haina tofauti sana na burudani za
kikristo kama kwenye kumbi za
starehe. Watu huwa wanaangalia tu,
lakini je, wanaabudu? Uwepo wa
Mungu na Roho wake katika ibada
zetu utawafanya watu wasioamini
kuanguka chini na kuabudu (Kol
3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe
5:19) (Mdo 2:4).
Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka
za kusifu. Daudi alicheza mbele za
Bwana kwa nguvu zake zote, na
akakataa kumtolea Mungu kafara
ambayo isingemgharimu cho chote
(2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi
wa Mashariki walitoa zawadi za
gharama kubwa walipokuja
kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na
mwanamke mmoja alimpaka Yesu
kwa mafuta ya gharama kubwa,
akamwosha miguu yake kwa
machozi yake, na kuifuta kwa nywele
zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada
yoyote inaambatana na kutoa tena
vitu vyetu vya thamani.
Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi
alivyo na kwa matendo yake; lakini
Mungu mwenyewe anawatafuta na
anawataka wafanya ibada, na si
mradi ibada tu. Kusifu kwaweza
kufanywa hadharani, lakini ibada
mara zote ni jambo la ndani ya
moyo. Kusifu mara zote kunaweza
kuonekana au kusikika, lakini
kuabudu yaweza kuwa ya
kimyakimya na iliyofichika. Kusifu
kunaonekana, kuna kutumia nguvu,
kuna misisimko na furaha; lakini
ibada mara zote ni heshima na hofu
katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi
Mungu anavyo hitaji na kutamani
kuabudiwa na yeye pekee yake
ndiyo anayestahili kuabudiwa.
Kusifu na kuabudu kwa siku za
leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa
mafundisho katika kusifu na kuabudu
na ndiyo maana ya kuanda somo hili
ili tupanuane mawazo. Watu wengi
wa leo wanadhani kusifu ni kuimba
kwa nyimbo zenye midundo ya
harakaharaka(zouk&sebene) na
ukipunguza spidi ndo kuabudu.
Hasha tunaposema kusifu inatokana
na maneno yaliyopon kwenye
wimbo husika kweli ni ya kusifu,
kama ni maneno ya kusifu tunasema
ni wimbo wa sifa haijarishi speed
inayotumika na hali kadhalika
nyimbo za kuabudu. Watu katika
kipengele hiki huwa wanachakanya
nyimbo utakuta wakati wa kusifu
anaimba wimbo wa kutia moyo au
wa maombi, kinachotakiwa ni kujua
kuwa kila jambo lina wakati wake
ziiko nyimbo za mazishi, kufariji,
kutia moyo, za maombi, za kusifu ,
na za kuabudu nk sasa usichanganye
kwenye kusifu wewe unaimba
parapanda italia au tuonane
paradiso, hizo sio za sifa sasa najua
wewe utafanya zoezi la nyimbo
unazozijua ili kufahamu zina ujumbe
gani na ziko katika kundi lipi kati ya
hayo niliyokufundisha hapo juu.
Baadhi ya maandiko yanayo
onyesha aina za kusifu na
kuabudu kwa:
1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)
2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)
3. Kuinama au kupiga magoti (Zab
95:6)
4. Kupiga makofi (Zab 7:1)
5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam
6:14)
6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)
7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law
23:40)
8. Kutembea (2Nya 20:21-22)
9. Shangwe (Zab 95:1)
10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law
9:23-24)
11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1,
32:11)
12. Ukimya (Mhu 3:7)
13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab
42:4)
14. Kulia/ kutoa machozi katika roho
mtakatifu
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza
ufalme wake na haki yake na hayo
mengine mtazidishiwa.

VIFUNGO VYA TABIA


Na Mch. Josephat Gwajima 04.03.2013



Utangulizi:
Shetani hajabadilika na silaha zake ni zilezile; na jambo kubwa linaloshangaza watu ni kwamba silaha za shetani ni zilezile lakini bado zinatenda kazi kwenye maisha ya watu. Moja ya kifungo kinachosumbua watu ni kifungo cha tabia.

Mara nyingi kupata urafiki au uhusiano ni rahisi lakini ili uweze kuendelea kuwa karibu na watu hao unatakiwa uwe na tabia nzuri. Hivyo shetani anaweza kukuacha usonge mbele na kazi ya Mungu lakini akakuzuia kupitia vifungo vya tabia. Kwasababu hii Roho Mtakatifu ametaka leo tujifunze kuhusu vifungo vya tabia:

KIPAWA NA TABIA YA MTU:
Kuna vitu kadhaa vya kuangalia kama mtu wa Mungu unayehitaji kufanikiwa, cha kwanza ni kipawa na pili ni tabia ya mtu.

Mithali 18:16 “zawadi ya mtu humpatia nafasi, humleta mbele ya watu wakuu; ” hili neno zawadi kwenye Biblia ya kingereza linaitwa “GIFT” au kwa Kiswahili kipawa. Sasa basi kipawa cha mtu chaweza kumfikisha mbele za watu wakubwa na kujulikana. Mfano mtu anaweza kuwa na kipawa cha uwimbaji lakini anakaa kijijini na umaskini, ila kile kipawa chake kikionekana kinaweza kumleta mtu huyo mjini hii ndio maana ya sehemu ya kwanza ya andiko hilo. Kwasababu hiyo kila mtu aliyepo duniani amepewa kipawa na Mungu ambacho kwa hicho anaweza kufika kwenye hatua ya juu zaidi.

Sasa basi kipawa cha mtu humleta mtu kwenye mafanikio yake, tatizo linakuja pale mtu anapokuwa na kipawa lakini tabia yake si nzuri. Hivyo tabia ndio ambayo inakubakiza katika sehemu uliyopo. Mtu anaweza kuwa na macho ya rohoni au upako lakini kama tabia yake ni mbaya hakuna mtu atakayetamani kuwa karibu naye. Ili Mungu akutumie kwa kiwango cha juu ni muhimu kuanza kwa kubadili tabia yako.

TABIA ZA KIMUNGU NA TABIA ZA ASILI:
Biblia imeainisha tabia za aina mbili, yaani tabia ya Kimungu na tabia ya kiasili au ya mwilini. Katika 1Wakoritho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.” 1Wakorintho 3:1 kuna tabia za rohoni na tabia za mwilini. Hivyo anachosema Mtume Paulo ni kwamba unapoongea na watu inabidi ujue ama mtu huyo ana tabia za rohoni au za mwilini. Mfano mtu anaweza kuwa mwimbaji mzuri lakini ana tabia ya uongo; Mtu mwingine anaweza kuwa na kipawa kitakachomfanya apate mchumba; lakini kama tabia yake ni mbaya ama uongo, au umbeya au uzinzi inaweza kumfanya kuachwa na mchumba wake sio kwasababu hapendwi bali kwasababu ya tabia. Tabia ya Kimungu ni tabia njema na nzuri lakini tabia ya kibinadamu ni tabia mbaya aliyonayo mtu.

Shetani akitaka kuharibu kipawa cha mtu anaanzia kwenye tabia yake; kwa maana hiyo tabia ya kibanadamu au ya mwilini ndio hiyohiyo Biblia inaiita tabia ya kishetani. Ukisoma katika Yakobo 3:15 “Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani.” Unaona kumbe tabia mbaya ya kinadamu ndio hiyo inaitwa tabia ya kishetani. Mhubiri 10:1 “Mainzi mafu huvundisha marhamu ya mwuza marashi; Kadhalika upumbavu haba ni mzito kuliko hekima na heshima.” Hili ni neno la hekima la Mfalme Suleimani kusema mainzi wanaweza kuharibu marhamu nzuri; ikimaanisha unaweza kupata mpenyo katika maisha lakini tabia mbaya inaweza kukupeleka mbali kabisa na upenyo wako.

Ndio maana waweza kumkuta mtu ni mwombaji au anatenda miujiza lakini tabia yake ikawa mbaya kwasababu ya asili. Jambo hili ndlo linalosabisha watu wengine kusema “kama ulokole ndio huu sitaki kuokoka” kumbe mtu huyo aliwahi kumuona mtu ambaye ameokoka na ananena au anaombea watu lakini ni mwongo au mzinzi. Katika Biblia, Samson alikuwa mnadhiri wa Mungu na alikuwa amepakwa mafuta tangu tumboni mwa mamaye. Japokuwa alikuwa mpakwa mafuta lakini alikuwa na tabia mbaya ya kutaka wasichana wa kifilisti ambao Mungu alikataza tangu mwanzo. Hii ni sawa na mtu kung’ang’ania kufungwa nira na mtu asiyeamini. Kwa njia hii Samson akakutana na Delila ambaye lengo lake halikuwa upendo bali ni kumharibia kipawa chake kwa kuijua siri yake. Vivyohivyo shetani amewaangamiza watu wa Mungu wengi kwa kuwafanya waoe au kuolewa na watu wasiomjua Kristo na matokeo yake kile kipawa cha Kimungu kilichokuwa ndani yao kinashindwa kuonekana tena.

KUBADILI TABIA:
Tabia mbaya ya mtu huondoka kwa kuamua mwenyewe, hata kama mchungaji akuombee mara zote kama tabia yako ni mbaya kwa asili inakulazimu kuamua kuibadili mwenyewe. Ni kweli tabia yako inaweza kuwa imeshakupotezea kibali kwa watu au imeshakupotezea upenyo katika maisha lakini ukiamua kuanza upya na BWANA na kuacha zile tabia mbaya Mungu wetu ni wa nafasi ya pili. Mungu wetu anatoa nafasi ya pili biblia inasema, “usifarahi ee adui yangu niangukapo mimi nitasimama tena”

Leo naongea na watu ambao walikuwa waombaji leo hawaombi tena, walimuhofu Mungu lakini leo hawana hofu, walikuwa watakatifu lakini leo ni waovu wakubwa Mungu anayo nafasi ya pili kwaajili yako. Amua kutubu na kuacha dhambi na tabia hiyo mbaya; Mungu atakuwezesha tena kama alivyomwezesha Samson kuwaangamiza wafilisti wote. Hivyo uamuzi wa kwanza ni kuamua mwenyewe kuacha tabia hiyo

VIFUNGO VYA MWILINI



Na Mch. Josephat Gwajima 03rd March, 2013


















Utangulizi:
Mungu anawapenda sana wanadamu na Biblia inasema wazi kuhusu hili katika kitabu cha Maombolezo 3:31; Ni raha yake kuona hatuna matatizo na tunaishi kwa amani. Mungu hakumuumba mwanadamu ateseke bali alimuumba afanikiwe akiwa duniani na kuishi kwa furaha.

Wakati huohuo, shetani kwa asili hapendi mtu aliyeumbwa na Mungu afanikiwe na ndio maana katika Luka 3:16 inasema, “…ambaye shetani amemfunga miaka kumi na minane…” (Matendo 10:38; 2Wathesalonike 2:18-19) kwa maandiko hayo tunaweza kujua kuwa shetani anaweza kufunga, kuzuia, kupinga na kushindana na mtu. Kwa asili shetani ni mshindani na furaha yake ni kuwatesa wanadamu ambao wanapendwa na Mungu. Yeye hufanya hivi ili kuumiza moyo wa Mungu kupitia wanadamu walioumbwa na Mungu.

SHETANI ANAWEZA KUMFUNGA MTU:
Kama tulivyoona kuwa shetani anapenda kuwatesa wanadamu na ili kutimiza lengo lake njia mojawapo anayotumia ni kuwafunga watu. Na tunapotaja vifungo, tunakuwa tunazungumzia vifungo vya aina kuu tatu, yaani, Vifungo vya mwilini, Vifungo vya rohoni na vifungo vya nafsini kwasababu mtu ni roho inayokaa ndani ya nyumba iitwayo mwili. Katika hatua hii ya kwanza tunaanza kuangalia kwa undani kuhusu vifungo vya mwilini:-

Mwili ni nini?
Hatuwezi kujua namna mwili unavyoweza kufungwa bila kujua asili ya mwili wa binadamu. Tuanze kwa kuangalia andiko hili Mwanzo 2:7 “BWANA Mungu akamfanya mtu kutoka katika mavumbi ya ardhi…” kumbe asili ya mwili wa mwanadamu ni mavumbi au udongo. Na ndio maana katika Isaya 64:8 Biblia inasema, “… sisi tu udongo nawe ni mfinyanzi wetu...” nabii Isaya ambaye aliwahi kumuona Mungu lakini alijua ukweli huu kuwa mwili ni mavumbi (Ayubu 7:21, 34:15). Kumbe pamoja na kuwa umevaa vizuri au umeupamba mwili vizuri lakini asili yake ni udongo na katika ulimwengu wa roho huonekana kuwa ni udongo kabisa. Kwa ufupi mwili wa mwanadamu ni udongo na mtu anapokufa mwili huirudia nchi (Mhubiri 12:7) yaani mavumbi.

Ndio maana hata watu wanapooana ni miili ndio ambayo inakuwa imeoana na si roho kwasababu mbinguni hakuna kuoa wala kuoana kule ni katika roho. Kwa kujua kuwa mwili ni udongo basi namna ambayo unaweza kuutendea udongo wa kawaida ndivyo vilevile waweza kuutendea mwili wa binadamu. Udongo wa ardhini waweza kuoteshwa mimea na kuchimbwa, vilevile na mwili wa binadamu waweza kufanyiwa hivyo.

TOFAUTI KATI YA MWILI NA UDONGO WA KAWAIDA:

Kuna mambo mawili makuu yanayosababisha mwili wa binadamu uwe tofauti na udongo wa kawaida.

1. Mwili uliwahi kushikwa na mikono ya Mungu maana hakuna kitu kilichowahi kushikwa na Mungu na kikabaki kama kilivyo.

2. Ndani ya mwili wa mwanadamu kuna roho ambayo huuisha mwili na kuupa uhai. Kwasababu hizo mwili wa mwanadamu hutofautina na udongo wa kawaida.

MWILI WA MWANADAMU UNAWEZA KUPANDIWA VITU:
Biblia iko wazi kuwa Mungu wa mbinguni anaweza kupanda, (Mwanzo 2:8); kumbe Mungu ambaye ni roho (Yohana 4:24) anaweza kupanda katika ardhi kabisa vivyo hivyo shetani naye ni roho naye ana uwezo wa kupanda katika mwili ambao kwa asili ni udongo. Hapa ndipo lile andiko la “KILA PANDO AMBALO BABA WA MBINGUNI HAKULIPANDA LITANG’OLEWA” linapoleta maana; Mapando ambayo hayajapandwa na Baba wa mbinguni ni lazima yatakuwa yamepandwa na shetani. Ndio maana ya mfano wa Yesu katika Mathayo 13:25 “lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.” Huyo ambaye Yesu anamwita adui ni shetani mwenyewe. Kumbe unapolala au kujisahau shetani huja na kupanda magugu, hili jambo linatendeka katika ulimwengu wa roho. Ni muhimu kujua siri hii kwamba kama vile udongo unavyopandwa vivyohivyo shetani naye anao uwezo wa kupanda juu ya mwili wa mwanadamu.

Unaweza kumsikia mtu analalamika kuwa mwili unachoma lakini kumbe katika ulimwengu wa roho mtu huyo amechomwa mkuki au kisu. Kufikia hapa sasa twaweza kujua kwanini Mungu alikataza kupanda mbegu mbili za tofauti katika shamba moja (Mambo ya Walawi 19:19). Mungu alisema hivi akitufundisha kuwa mahali ambapo Mungu amepanda shetani hatakiwi kupanda mahali pale. Mtu anaweza kuhisi vitu vinatembea mwilini kumbe amepandiwa wanyama wanaotembea katika mwili wake.

PEPO ANAWEZA KUJIGEUZA NA KUWA CHOCHOTE:
Tulijifunza kuhusu sheria mbili za rohoni, hapo tuliona uwezo wa pepo wachafu kujigeuza na kuwa kitu kingine yaani kuvaa sura mbali mbali ili kutimiza kazi zao. Jambo hili twaweza kuliona katika (1Wafalme 22:19-23) huyu pepo kwa asili hakuwa wa uongo lakini aliweza akaenda na akawa pepo wa uongo. Yule pepo akaingia katika vinywa vya manabii wa Mfalme Ahabu na kuwafanya wamtabirie uongo. Kwa maana hiyo tunaona uwezekano wa pepo mchafu kujigeuza na kuwa kitu chochote ili kutimiza lengo alilokusudia.

Sasa twaweza jua kuwa mapando tuliyokuwa tunayazungumzia ni pepo wachafu ambao hujigeuza na kuwa kile kitu na hivi ndivyo vinavyoitwa “Vifungo vya mwilini”. Wakati mwingine pepo anaweza kujigeuza na kuwa kinywa cha mtu, kama pepo wa katika (1wafalme 22:19-23) alivyofanya. Hivyo; unaweza kumuona mtu anatukana matusi ya ajabu bila hata aibu, kumbe pepo kajigeuza na kuwa kinywa chake. Pepo anaweza kuwa uso wa simba, unamkuta baba mwenye nyumba mkali kwa watoto na mkewe kumbe ni uso wa simba. Kwahiyo; pepo wanaweza kujigeuza maumbo mbalimbali kama nyani, simba, paka hata bundi ili mradi kuharibu hatma ya mtu. Mnamkuta dada aolewi kumbe uso wake umefunikwa kwa sura ya simba, kila mwanaume anayetaka kumchumbia haoni sura nzuri bali anaona simba. Na ndio maana kuna baadhi ya wadada watumia muda mwingi kujipodoa lakini bado hawapendezi kwa kuwa uso sio wa kwake.

KUNG’OA KILA KILICHOPANDWA KATIKA MWILI WAKO:
Imeandikwa kila pando asilolipanda Baba wa mbinguni litang’olewa, hivyo Mungu ametupa mamlaka ya kung’oa kila pando la kishetani yaliyopandwa katika mwili. Miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu hivyo shetani hatakiwi kugusa sehemu yoyote ya mwili wako.

Tumia mamlaka yako kung’oa kila pando ambalo shetani amepanda katika maisha yako mapando ya magonjwa, homa zisizoisha, ukimwi, mwasho wa mwili na matatizo mbalimbali. Jina la Yesu lina mamlaka yote dhidi ya kazi zote za shetani katika maisha yako.

Tuesday, February 5, 2013

MAOMBI YANAYOZAA MATUNDA

Na-
MCHUNGAJI: FRANK ANDREW (RP)

UTANGULIZI:

Mungu anatuhitaji tuombe, tunatakiwa
tuombe sio tu kwasababu tunauhitaji
bali kwasababu Mungu anahitaji tuombe.
Tatizo la watu wengi wanashindwa
kupokea majibu ya maombi
wanayoomba na wengine wameshindwa
hata kuomba.wengine wamejikuta
wakikata tama bila kujua kuwa wao ndio
wanakosea katika kupeleka haja zao kwa
Mungu na katika kupokea. Hapa
tutajifunza sababu na jinsi ya kuomba ili
kupokea kutoka kwa BWANA.

SABABU NNE: KWANINI
TUNAMUOMBA MUNGU:

1. Kujinyenyekesha mbele za Mungu.
2. Kuonyesha kuwa yeye ni Mungu
wetu.
3. kuonyesha kuwa vyote viko mikononi
mwake
4. Tunampa heshima kama baba
mwenye familia ya watoto watakatifu.

MAOMBI YANAHUSISHA VITU
VIKUBWA VITATU:

1. Mhusika AU muombaji mwenyewe:-
huyu ndiye muombaji na mwanzilishi wa
maombi.
2. Maombi yenyewe:- haya ni mahitaji
au ujumbe ambao unapelekwa kwa
unaye muomba.
3. Unayemuomba:- unayemuomba ni
nani kwako na mna uhusiano gani naye.
Kwa kujua umuhimu wa kuomba,
wanafunzi wa Yesu walimwomba Yesu;
awafundishe jinsi kuomba na hapo Yesu
aliwapa fomula ya kuitumia ili kuomba.
Hii ndiyo inayoitwa sala ya BWANA,
kimsingi hii ni kanuni ya kuomba
aliyoifundisha Yesu na si maombi
yenyewe kama wengi wanavyodhani,

KANUNI hii ni sawa na kanuni yengine za
kufanya jambo fulani. Mfano kuna
kanuni za kupika au kanuni za kuimba.
Tatizo la watu wengi ni kwamba
wanatumia hii kanuni kama ndio
maombi yenyewe. Kwa mfano Yesu
aliposema “Baba yetu uliye mbinguni…”
alimaanisha kuwa unapokuwa unaanza
kuomba ni lazima ujue unamuomba
baba aliye mbinguni na si magomeni. Hii
ni kanuni jinsi ya kuomba na haitaji moja
kwa moja haja yako, bali ukiitumia kama
kanuni inakuletea majibu:=

Yakobo 5: 15-16 “kuomba kwake
mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa
bidii”, Biblia inaposema kuomba kwake
mwenye haki: anamaanisha kuwa yeye
anayeanzisha maombi ni lazima awe ni
mwenye haki yaani msafi. Kiukweli kuna
wakati mwingine Mungu hutenda
kwasababu ya neema yake lakini
kimsingi ili maombi yako yafae inabidi
uwe mwenye haki. Hivyo kabla ya
kuingia kwenye maombi unatakiwa
ujitakase kwanza ili Mungu akikutazama
aone uko safi. Ni muhimu kutengeneza
uhusiano mzuri na Mungu, tengeneza
haki kwanza kabla ya kuingia kwenye
maombi. Yaani kama hujaokoka uokoke
kwanza, na kama umeokoka lakini hauko
sawa na Mungu, unatakiwa utengeneze
maisha yako kwanza. Katika mstari wa
15* Biblia inasema “ungameni dhambi
zenu ninyi kwa ninyi” ikiimaanisha kuwa
kabla ya kuingia kwenye maombi
unatakiwa ujisafishe na ujitakase
kwanza.
Baada ya kujitakasa kinachofuata ni
kupeleka ujumbe wenyewe kwa Mungu.
Watu wengi kwasababu hukosea kuomba
wamedhania kuwa Mungu huwa hajibu
maombi; lakini Biblia inasema Mungu
anajibu maombi. Biblia inasema, Zaburi
2:8 “uniombe nami nitakupa mataifa
kuwa urithi wako...” na katika Mathayo
7:7 “Ombeni nayi mtapewa…” kumbe
unapoomba lazima Mungu akujibu kama
ukiomba sawasawa na mapenzi yake. Ni
muhimu kabla ya kupeleka hoja yako
uamini kwanza kuwa Mungu yupo
sawasawa na Waebrania 11:6 “...lazima
aamini kuwa Mungu yupo”. Haya
maandiko tutatumia katika kuangalia
jinsi ya kuomba na wapi watu wengi
wanapokosea wakiwa katika kuomba…

KANUNI ZA KUPOKEA KUTOKA KWA
MUNGU:

Watu wengi wanajua kuomba lakini kati
yao wengi hawajajua namna ya kupokea.
Kwasababu kuna namna ya kuomba na
namna ya kupokea. Watu wengine
wanajua kuomba lakini hawajui jinsi ya
kupokea haja zao. Haifaidii kitu kujua
kuomba na huku ukiwa hujui jinsi ya
kupokea. Kuna mambo kadhaa ambayo
unatakiwa uyatilie maanani unapokuwa
unaomba kama ifuatavyo:-

1. Tengeneza uhusiano wako na
Mungu:-
Maandiko yanasema “haja zenu na
zijulikane mbele za Mungu” pamoja na
kuwa Mungu anajua haja zetu lakini bado
anahitaji sisi tumuombe. Hii ni sawa na
kuomba kwa jirani wakati baba yako
mzazi yupo; utajisikiaje mtoto wako
anapokuwa na shida alafu akuombi
wewe baba yake, alafu yeye
anajitengenezea sanamu na kuiomba.
Utakavyojisikia ni sawa kabisa na Mungu
anavyojisikia kwetu ndio maana Mungu
anasema kuwa anaona wivu (kutoka
20:4) . Mungu anataka tumuombe yeye
ili kujenga uhusiano na yeye. Ukiomba
au kuiabudu sanamu unamfanya Mungu
awe na wivu.

2. Unaongea nini ukiwa katika
maombi yako:-
Maombi unayoongea kwenye maombi ni
ya muhimu sana kwenye kupokea haja
zako kutoka kwa BWANA. Ttuangalie
kwa habari ya Hana; 1Samweli1:1-24; Elikana alikuwa na wake wawili
Penina na Hana, kama lilivyojina lake
Hana hakuwa na watoto kwasababu
tumbo lake lilikuwa limefungwa. Hana
hapo kwanza alikuwa anaenda na
malalamiko na kulia. Watu wengi
hupeleka malalamiko kwa BWANA,
badala ya kupeleka hoja kwa Mungu.
Hata siku moja Mungu atendi jambo bila
kusudi, na ndio maana tumbo la Hana
lilikuwa limefungwa kwa muda wote ule.
Emu tuangalie mambo kadhaa
yaliyokuwa yakimzuia Hana.
>Sababu ya kuomba:-
1Samweli 1:1-24 Hana alikuwa
anamuomba Mungu ampe mtoto ili
amkumeshe penina, na ndio sababu
inayowafanya wengi washindwe kupokea
kwa BWANA kwasababu hawana sababu
ya Kibiblia inayowafanya Mungu awape
mahitaji yao. Mfano mtu anamwomba
Mungu mke ili amfulie nguo au
amechoka kuishi mwenyewe. Hiyo si
sababu; Mungu anahitaji hoja yenye
nguvu ili upokee mwambie jukumu lako
la kutimiza kwenye maisha yako na
nafasi ya mke katika kumtumikia Mungu;
hapo lazima akutendee.

>Peleka haja ya moyo wako:-

Mungu haitaji hali yako ikoje sasa bali
anahitaji kujua unataka nini. Picha ya
tatizo lako unatakiwa uwe nayo wewe
lakini mbele za Mungu unatakiwa
upeleka haja ya moyo wako na si
malalamiko. Kwa wakati ule Hana
alikuwa anapeleka hali yake ilivyo na
penina na si uhitaji wake kwa BWANA.
Unakuta mtu anamuomba Mungu gari ili
awaonyeshe wengine, huyo hawezi pata
kwasababu si sawa na mapenzi ya
Mungu.

>Mwangalie Mungu na si jambo
unalohitaji:

Ibarahimu alipompokea Isaka
ilimradhimu Mungu kumjaribu ili ajue
upendo wake upo kwa Isaka au kwa
Mungu. Watu wengi wanamuomba
Mungu jambo lakini wakilipokea ndilo
linalofanyika mzigo mkubwa wa
kutokumtumikia Mungu, mfano mtu
anaomba mume akipokea tu; baada ya
siku chache haji kanisani anasema eti
anamuhudumia mumewe. Kwasababu
hii hata Hana akupata mtoto mpaka
alipobadilisha maombi na kumuomba
Mungu mtoto, kwa kumuahidi BWANA
kumtoa mtoto huyo awe mtumishi
wake.

3. Imani na Bidii:
Watu wengi wanafikiri bidii ni kutumia
nguvu tu katika maombi, bali bidii ni ule
mzigo; ni muhimu unapokuwa unaomba
uwe na mzigo wa kuombea. Ili uzae
matunda katika maombi ni lazima uwe
sawa na mama mjauzito aliye katika
kuzaa; lazima uwe na uchungu yaani
umaanishe. Vivyohivyo kupokea kutoka
kwa BWANA Unatakiwa umaanishe na
lazima uamini pia kuwa ni wakati wako
wa kupokea kutoka kwa BWANA.
Unapoomba unatakiwa moyo na akili
yako iwe kwenye kile unachohitaji. Kuna
watu wanabidili maombi kila kukicha kwa
kuhisi kuwa Mungu awasikii lakini bidii ni
kubaki kwenye jambo hilo hadi uone
amani moyoni kuwa BWANA
ameshatenda na hili jambo ndilo ambalo
Eliya alilifanya alipokuwa anaomba mvua
kunyesha tena. Eliya alikuwa
mwanadamu wa namna moja na sisi
alikuwa na Bidii katika maombi.

JAMBO LA KUFANYA:

Baada ya kujua mambo haya ni muhimu
kubadili mtazamo wako na jinsi
unavyoomba. Mungu anajibu maombi
kama ukiomba sawasawa na neon lake.
Kwanza uwe na picha ya kile ambacho
unataka BWANA akutendee, uombe na
imani na bidii. Hapo lazima Mungu
akutendee kwasababu hakuna baba
ambaye mwanaye atamwomba mkate
akampa jiwe au samaki akampa nyoka.
Badili mtazamo wako katika maombi
yako ili uwe mpokeaji wa maombi yako
ni si mwombaji asiyepokea chochote!!!

-FRANK ANDREW-
Resident Pastor G.C.T.C

Sunday, February 3, 2013

WAKATI UFAAO KUANDAA SILAHA YAKO.

Na; CONRAD CONWELL
Silaha hutengenezwa wakati wa
amani,wakati wa vita ndipo
hutumika....."WAKRISTO wengi wakati wa
amani hawaombi,ila mambo yakigeuka
kidogo hufunga na kuomba,Wakati wa
kuzama si wakati wa kujifunza kuogelea bali
ulipaswa kujifunza kabla,fanya maazimio ya
kumtafuta MUNGU wako siku za amani na
simama kwenye zamu yako
kikamilifu,Mtafute Mungu wako kwa Bidii...
Mithali 8:17
Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Andaa na uvae silaha
sasa,
Luka 21:34-36.
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima. Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.
"BWANA MUNGU AWABARIKI NA KUWAPA NGUVU ILI KUWEZA KUANDAA SILAHA "

MATUKIO YA KICHAWI (sehemu ya pili)

UTANGULIZI:
Watu wengi wanajiuliza kwanini
tunazungumzia uchawi mara nyingi, hii ni
kwasababu shetani hutumia wachawi
katika kutenda kazi duniani; na ndio
maana katika Biblia kuna maandiko
mengi yanayotaja uchawi na wachawi
kama ifuatavyo:- Hesabu 23:23 24:1;
1Wafalme 9:22; 2Wafalme 17:17;
Isaya 47:9,12; Mika 1:12; Nahumu
3:4; Matendo ya Mitume 8:9; 18:11;
Wagalatia 5:20; 3:1; Ufu 9:21. Ni kweli
tumepewa mambo yote na Mungu kama
vile afya na mafanikio lakini shetani
kupitia wachawi amekuwa akizuia, hivyo
tunatakiwa kushughulika nao katika
ulimwengu wa roho.. Katika sehemu ya
kwanza ya somo hili tuliona kwa habari
ya Ayubu ambapo shetani alipata ruhusa
ya kugusa maisha yake. Shetani
hakumtokea Ayubu kwa namna ambayo
angemfahamu kuwa ni shetani, lakini
alimjia kwa njia ya matukio, kumbe
waweza kuwa unapitia kwenye hali
mbaya kumbe ni matukio
yanayosababishwa na wachawi.
Wakristo walio wengi wanapambana na
shetani bila kujua nguvu za adui wanae
pamaba nae. Nchi ya Japani ilipokuwa
haijui kuwa Marekani wana bomu la
nyuklia; waliwachokoza wakidhania kuwa
watashinda, Lakini matokeo yake
walishindwa kwasababu walikuwa
hawajui nguvu ya wanayeshindana naye.
Mara nyingi watu wengi hupambana na
shetani bila kujua nguvu zake na
matokeo yake wengi huishia kushindwa.
Huwezi kupambana na adui usiyemjua,
vivyohivyo ili uweze kumshinda shetani
ni lazima uanze kwa kutafuta maarifa
kuhusu yeye.
MAFURIKO YA KICHAWI:
Ufunuo 12:13-16 Yule Joka alikuwa
shetani, Biblia inasema Yule joka akatoa
maji kama mto; kwa kawaida
ingeonekana kama mafuriko ya maji
dhidi ya yule mwanamke. Kumbe kuna
matukio yanaweza kutokea kwenye
maisha yako au kwenye nchi, na kumbe
yamesababishwa na wachawi. Si kila
moto au mafuriko ni ya kiasili, mengi
huwa yanasababishwa na shetani ili
kuua watu ili awashushe kuzimu. Kuna
matukio yanatokea unadhania kuwa ni
ya kawaida kumbe yameletwa na
wachawi ili kuangamiza watu. Ni
muhimu kujifunza kuyaangalia matukio
kwa jicho la rohoni.
BIASHARA ZA KICHAWI:
Ezekieli 28:16, 18. “kwa wingi wa
uchuuzi wako; watu walikujaza
udhalimu” shetani mfanya biashara naye
hutenda kazi pamoja na wachawi na
waganga wa kienyeji. Kwa njia hii
shetani anafunga maisha ya watu, na
ndio maana kuna watu wanafanya
biashara za kichawi, Yaani
wanamwendea shetani halafu
wanamuomba aiwezeshe biashara yao
kwa kumpa shetani ama damu au
kafara. Wachawi wanapokuwa wanatoa
kafara, huwa wanakuwa wanafanya
biashara na shetani. Ufunuo 18:1-
mstari 5” “wafanya biashara wa nchi
wamepata mali kwasababu ya kiburi
chake” mstari 11” “nao wafanya
biashara wa nchi walia na kuomboleza
maana hapana mtu anunuaye bidhaa zao
tena” mstari 13 ” biashara ya roho na
miili ya wanadamu. Kumbe biashara
nyingi unazoona watu wanafanya
duniani, ni biashara za kichawi. Yaani
mtu anafanya biashara lakini ndani yake
kuna uvuvio wa kishetani, Nahumu 3 : 4 .
Ndio maana biashara za watu wengi
hazifanikiwi wakati huohuo watu
wanaomtegemea shetani wanafanikiwa
kwa haraka ni kwasababu wameuza roho
zao kwa shetani.
Matendo ya Mitume 16:16-17; 19:24
“aliyewapatia bwana zake faida nyingi”
biashara hizi zipo kabisa, na ndio maana
unaweza kufanya biashara lakini
wenzako wanauza zaidi kuliko wewe
hata kama wote mnauza bidhaa ileile,
kumbe wenzako wamenuiza ili wao
wauze na wewe usiuze. Ni vizuri kuanza
kufanyabiashara na BWANA, yaani kabla
ya kuanza biashara ni muhimu kufanya
maombi kwanza ili kuiweka biashara
yako katika ulinzi wa Mungu. Unapotaka
kuanza biashara fanya na BWANA.
MAGONJWA YA KISHETANI:
Kuna watu ni wagonjwa sasa kwasababu
ya wachawi. Magonjwa mengi sana
husababishwa na wachawi. Unaweza
kuwa unasumbuliwa na magonjwa
yasiyopona kwasababu ya chanzo chake
ni cha rohoni. Na ndio maana
unapooumwa hata kama utaenda
hospitali unatakiwa usiache maombi
kwasababu shetani anaweza kusababisha
magonjwa, hata Ayubu aliumwa majipu
mabaya ambayo kimsingi yalisababishwa
na shetani.
BIBLIA NA MATUKIO YA KICHAWI:
Mathayo 9:32 “tazama walimletea mtu
bubu mwenye pepo, na yule pepo
alipotolewa alinena” huyu ni mtu
ambaye watu walipomuangalia
walimuona ni bubu. Cha ajabu Yesu
alipomuona hakushughulika na ububu
bali alishughilika na pepo kuonyesha
kwamba ule ububu ulisababishwa na
pepo. Kuna mambo mengi ambayo
yanasababishwa na shetani, hivyo
unatakiwa kuyashughulikia.
Mathayo 13:10-15 “alikuwa na pepo wa
udhaifu kwa muda wa miaka kumi na
nane…” 15” “na huyu mwanamke aliye
uzao wa Ibrahimu ambaye shetani
shetani amemfunga” watu walishamzoea
kumwona kuwa ni mama mwenye
kibiyongo yaani hawezi kujinyoosha
kabisa lakini Yesu alipomtoa pepo Yule
mama alipona.
Wachawi wapo na watu wengi
wanalogwa, Kumbukumbu la Torati
18:11 ; watu wanalogwa na wanalogeka,
matatizo ya watu wengi yanasababishwa
na shetani kupitia matukio ya kichawi.
Marko 9:17 ; kuna magonjwa ambayo
yanakuja kwenye maisha ya mtu
kwasababu ya kulogwa. Katika utendaji
kazi wa shetani anaweza akaingia ndani
ya mtu na kumfunga, lakini pia shetani
anaweza kumkandamiza mtu akiwa nje
ya mwili na ndio maana kwa watu
waliokoka lakini hawapigani vita ya
rohoni wanaweza kujikuta
wanakandamizwa na shetani akiwa nje
yao. 1Wathesalonike 2:18 , Paulo
hakuwa amepagawa na pepo lakini
shetani alimzuia. Zekaria 3:1 . Shetani
anaweza kukuzuia kutokea nje, yaani
unahitaji kwenda nje ya nchi lakini
shetani anakuzuia kupitia mtoa pasi ya
kusafiria. Matendo ya Mitume 13:6
hata wachawi hupambana pia ili
kukuzuia, ni muhimu kuishi maisha huku
ukijua kunakushindana rohoni.
JINSI YA KUSHINDA DHIDI YA
MATUKIO YA KICHAWI
Mpokee Yesu kwanza; huwezi
kushindana na shetani kama hujaokoka,
ni muhimu umpokee Yesu kwanza ili
akuwezeshe kupigana katika vita dhidi ya
shetani. Jifunze kuomba mwenyewe;
baada ya kuokoka kuna amani ya
mwanzo unayoipata ile isikufanye
ukasahau kuwa tupo vitani, kama
tulivyoona hapo juu wanaoshindana
nawe wanaweza kuwa ndani yako au nje
yako. Katika hali hiyo unachotakiwa
kufanya ni kujifunza kuomba mwenyewe
kwasababu hata ukitegemea kuombewa
kila siku, kuna muda utakuwa
mwenyewe, na hapo unatakiwa
usimame mwenyewe. Mtu uliyeokoka
unatakiwa uhame kwenye ule wokovu
wa kuombewa uhamie kwenye wokovu
wa maarifa na kupambana kwa kutumia
Jina la Yesu Kristo.

Sunday, January 27, 2013

MATUKIO YA KICHAWI

Na Mch. Kiongozi: Josephat Gwajima
Jumapili 27 th
January 2013

Kuna matukio ambayo yanaweza
kutokea kwenye maisha yako na ukaona
kuwa ni kawaida, lakini tambua kuwa
matukio mengi huanzia rohoni. Matukio
ya kishetani yanayoanzia rohoni
yanaitwa matukio ya Kichawi. Tutajifunza
somo hili kwa kuangalia kwa undani
kuhusu Ayubu. Ayubu 1:1-... ; kitabu
cha Ayubu kinaanza kwa kusema
palikuwa na mtu mmoja katika nchi ya
Usi…. Ayubu alikuwa anamcha BWANA,
si mwenye dhambi…
Shetani akamwambia Mungu
umembariki Ayubu ndio maana
anakucha wewe, Mungu akamwambia,
Katika Mstari wa 12’ “tazama yote
aliyonayo yapo mikononi mwako lakini
usinyooshe mkono juu yake mwenyewe”
jambo la ajabu linatokea, mara tu baada
ya Mungu kumruhusu shetani, jambo la
kwanza shetani alianza kwa kuharibu
mali zake (Ayubu 1:13…). Na katika kila
tukio alilofanya shetani, alibakisha mtu
mmoja wa kumpelekea habari Ayubu.
Hii ni kwasababu shetani alitaka Ayubu
asijue kuwa ni shetani bali Waseba ndio
walioua na kuchukua mifugo wake ili
amuhamishe mtazamo asifahamu kuwa
ni jambo la kishetani,ndivyo amabavyo
shetani anatenda kazi ahata leo.
Tukio la kwanza, Ayubu 1:13-15 Waseba
waliwavamia watumishi wa Ayubu,
unaweza ukawachunguza Waseba katika
mitazamo miwili. Upande mmoja ni
kwamba waseba ni mashetani waliovaa
miili au ni watu walioingiliwa na mapepo
kuharibu wanyama wa Ayubu. Tukio la
pili limetajwa katika mstari wa 16’
kwamba moto ulishuka kutoka
mbinguni, mtoa taarifa anaita moto wa
Mungu, lakini katika kitabu cha (Ufunuo
13:13) inasema shetani anaweza
kushusha moto pia. Huyu mfanya kazi
aliita moto wa Mungu ili kwa njia hiyo
shetani amdanganye Ayubu aache
kuangalia shetani bali awaze kuwa ni
matukio ya kawaida kutokea. Ndio
maana katika waebrani 11:34 , biblia
inasema kwa imani walizima nguvu za
moto, kwasababu kuna moto ambao
waweza kuletwa na shetani. Haijalishi
unapitia moto gani kwenye maisha yako,
moto wa mikosi, kushindwa, umaskini na
kila moto wa maisha yako uzime katika
Jina la Yesu Kristo usiite ni matukio ya
asili.
Tukio la tatu linawahusu Wakaldayo,
katika mstari 17’ wameunda vikosi vitatu
vitatu, nao ni watu ambao
wameandaliwa na shetani ili kutekeleza
yale maongezi ya mwanzo ya Mungu na
shetani. Kumbe ni muhimu kuangalia
matukio kwa namna ya rohoni, liwe
tukio la kukosa umeme au nchi kuwa
maskini liangalie kwa namna ya rohoni.
Nguvu ya shetani ni kukufanya uwaze
kuwa ni tukio la kawaida au la kiasili
lakini kumbe kuna nguvu ya shetani
nyuma yake. Tukio la nne ni upepo
uliotokea na kuangusha nyumba
waliokuwepo watoto wa Ayubu
waliokuwa kwenye sherehe. Cha ajabu
ni kwamba watoto wote wa Ayubu
walikufa kwa maana ndio walikuwa
walengwa,ila Yule mtoa taarifa hakufa
kwasababu si mtoto wa Ayubu na pia
hakuwa amelengwa yeye. Kumbe
unaweza kuwepo mtego wa kichawi nao
unakuwa umemlenga mtu husika, na
ndio maana katika Biblia inataja mitego
ya ibilisi, yaani ibilisi anaweza kumtega
mtu katika kitabu 2Timotheo 2:26
“wapate tena fahamu zao, na kutoka
katika mtego wa ibilisi…..” hivyo alikuwa
anabakishwa mmoja kwasababu lile tego
halimuhusu, maana tego humlenga mtu
au watu husika.
Usione ni kawaida, matukio kama hayo
yanapotokea katika maisha yako, mfano,
unaanza saluni halafu haifanikiwi kumbe
ni kwasababu ya shetani, cha kufanya
unatakiwa uingie rohoni kushughulikia.
Pigo la Ayubu kubwa la kumwekea
majipu katika mwili na magojwa,
unaweza kuhangaika hospitali kama
hujajua kuwa kimeanzia rohoni, hospitali
wataita jipu au cancer lakini kumbe
limeanzia rohoni. Na ndio maana
unaweza kuona meli zinazama hadi
hazionekani kumbe ni kazi za adui
shetani, ni muhimu kujua kila unapoona
matukio duniani kuna matukio ya
kishetani ama yameletwa na shetani au
yamesukumwa kuwepo na shetani. Na
ndio maana ni muhimu unapoingia
kwenye hatari au ajali ukailiitia Jina la
Yesu ambalo ndilo pekee tulilopewa
kuokolewa kwalo.
1Thesalonike 2:18 “ Nalitaka kuja
kwenu….. lakini shetani akatuzuia”
shetani anaweza kumzuia mtu, na mara
nyingi kwenye kuzuia shetani hutumia
watu wa kawaida ili usimtambue.
Huwezi kukutana naye macho kwa
macho kwasababu anatumia waseba,
wakaldayo au upepo. Na ndio maana
unaweza ukawa unataka kusafiri lakini
ukazuiwa na mtu anayetakiwa akupe
viza. Ni muhimu kujifunza kuangalia
matukio kwa jicho la rohoni. Kwasababu
kama hujui waweza kumchukia mtu,
kumbe shetani ndio yupo ndani ya mtu
anayekuzuia. Matendo ya Mitume
10:38 , Shetani anaweza kumuonea mtu,
pia anaweza kumwingia mtu maana
aliwahi kuingia ndani ya Yuda, na wakati
huo usijue kuwa ni shetani kumbe
anatumia mtu. Kabla hujapambana na
mtu anza na rohoni kwanza.
Luka 13:16 “…ambaye shetani
amemfunga…” kumbe shetani anaweza
kumfunga mtu, mapato, ndoto,
matumaini au mafanikio. Unapomtaja
shetani lazima ujue kuwa ana watumishi
wake. Mungu ana watoto wake na
shetani pia ana watoto wake, wale
wanaotenda mapenzi ya shetani ni
watoto wa ibilisi 1Yohana 3:10. Yohana
8:44 “…ninyi ni wa baba yenu ibilisi….”
Wachawi na waganga ni wana wa ibilisi
hivyo hitekeleza kazi za ibilisi duniani,
na hawa ndio wanaoleta matukio
mbalimbali. Shatani hushambulia eneo
ambalo Mungu amekubarikia, ili
usilitumie kukuletea mafanikio kwenye
maisha yako.
Jambo la Muhimu ni kwamba; unatakiwa
uangalie kila tukio linalotokea katika
maisha yako kwa jicho la rohoni, matukio
mengi huanzia kwa wakala wa shetani
na wachawi. Jambo la muhimu ni kuwa
unapookoka unapokea mamlaka dhidi ya
shetani na wakala zake. Ni muhimu
kuchukua nafasi yako kushughulika na
shetani na wakala zake kwa njia ya
maombi (katika ulimwengu wa roho).
Ukifanikiwa kuharibu chanzo cha tatizo
unakuwa umemaliza tatizo asilimia mia
moja.

Saturday, January 26, 2013

MSIPOONGOKA NA KUWA KAMA VITOTO,HAMTAINGIA KAMWE KATIKA UFALME WA MBINGUNI. ( Mathayo 18 : 3 )

BWANA YESU ASIFIWEE.......

Nakukaribisha mpendwa katika Kristo
Yesu,tujifunze kwa pamoja kuuhusu
ujumbe huu wa leo,Na umekujia muda
sahihi kabisa ungali U mzima wa afya.
Nependa kutambua uwepo wa Roho
mtakatifu muda huu,Ninamualika Yeye
Roho wa Bwana achukue nafasi,ashuke na
uweza wake ili uelewe pindi usomapo
ujumbe huu,maana Yeye ndie mwalimu
wetu siku ya leo.
Hayo maneno yaliyobeba kichwa cha somo
letu ni maneno ya Bwana Yesu Kristo
alipokuwa anawaambia wanafunzi wake, Na
ni maneno ya msingi katika mchakato wa
kwenda mbinguni,Sasa twaweza kusoma ;
Mathayo 18 : 1-3
“ Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu
wakisema,
Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa
mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka
katikati yao,
akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka
na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe
katika ufalme wa mbinguni. ”
Waingiao katika ufalme wa mbinguni ni
wale wenye kufanana kama watoto
wadogo,maana hawa watoto siku zote wao
ni wanyenyekevu sana.
Kumbuka ;
Bwana Yesu Kristo alikuwa anaongea na
wanafunzi wake,wale ambao waliitao Jina
lake,wenye hofu na Mungu,Labda kwa leo
niseme Yesu anazungumza na wewe
uliyeokoka akikuambia USIPOONGOKA NA
KUWA KAMA MTOTO
MDOGO,HAUTAINGIA KAMWE KATIKA
UFALME WA MBINGUNI..
Yaani ingawa umeokoka lakini bado
kuokoka kwako hakukusaidii kuingia katika
ufalme wa mbinguni kama usipoongoka.
• JE KUONGOKA NI NINI ?
• JE KUNA TOFAUTI GANI KATI YA
KUONGOKA NA KUOKOKA ?
MAJIBU ;
Kuongoka ni kugeuka kwa mwenendo wako
wa kwanza na kufuta mwenendo mpya
baada ya kusikia neno la Mungu.
Tofauti kati ya kuongoka na kuokoka ni hii;
• Kuongoka sio NEEMA ya Mungu kwa yule
aliyeongoka,Bali ni jitihada zake pindi
anapoukulia wokovu. Baada ya kuokoka.
• Bali Kuokoka ni KIPAWA/NEEMA ya
Mungu mwenyewe kwa watu wake, Hapa
tunasoma Waefeso 2 : 8-9
“ Kwa maana mmeokolewa kwa neema,
kwa njia ya imani; ambayo hiyo
haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha
Mungu;
wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije
akajisifu. ”
Haleluyaa…
Sasa unaweza ukawa umeokoka lakini
haujaongoka,Yaani umepewa neema ya
kumkiri Bwana Yesu Kristo, kuwa Bwana na
mwokozi wa maisha yako,na kuitwa
MLOKOLE katika jamii ulipo werwe,
lakini ujabadilika matendo yako yale ya
mwanzo kabla ya kuokoka yaani kama ni
WIZI unaufanya kidogo chini kwa chini,au
kama ni UZINZI pia unaufanya chini kwa
chini,na MTU YEYOTE WA NAMNA
HII,HUYO BADO HAJAONGOKA NA KAMWE
HATAINGIA KATIKA UFALME WA
MBINGUNI.
Mfano wa kuongoka;
Tumtizame mtume Paulo namna
alivyokuwa kabla ya kuongoka;
MATENDO 22 : 1-4
“ Enyi wanaume, ndugu zangu na baba
zangu, nisikilizeni, nikijitetea mbele yenu
sasa.
Waliposikia kwamba anasema nao kwa
lugha ya Kiebrania wakazidi kunyamaza;
akasema,
Mimi ni mtu wa Kiyahudi, nalizaliwa Tarso,
mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu,
miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria
ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu wa
jitihadi kwa Mungu kama ninyi nyote
mlivyo leo hivi;
nikawaudhi watu wa Njia hii hata kuwaua,
nikawafunga, nikiwatia gerezani, wanaume
na wanawake. ”
Hapo Paulo anasimulia kwa kujitetea
akiwaambia Wayahudi namna
alivyokuwepo hapo awali,lakini pindi
alipookolewa na Bwana Yesu na kutengwa
kwa dhumuni maalumu la kuwa mtume na
mjumbe wa Yesu Kristo,Ndipo
akaongoka,yaani akabadili ule mwenendo
wake wa awali wa kuwahudhi wakristo,na
kuwa mpya kwa ajili ya kazi ya Bwana.
Sasa siku hizi kuna kundi kumbwa la watu
waliokoka kama fasion lakini
HAWAJAONGOKA NA KUWA KAMA
WATOTO WADOGO na watu hayo
nawatangazia kwamba HAWATAUONA
UFALME WA MBINGUNI.
JE NI KWA NINI BWANA YESU ATUMIE
MFANO WA WATOTO KATIKA KUONGOKA?
MAJIBU ;
Kwa sababu watoto wadogo ni wale wenye
KUTII ,na sifa kama,na kuwa na sifa kama
zifuatazo ;
• Watoto wadogo usikia na kushika kile
wanachoambiwa bila kuhoji hoji
• Watoto wadogo hucheza na wenzao kwa
kushirikiana bila kuulizana kabila zao wala
hata majina yao .MFANO ;
wanapocheza wote wanakuwa ni wamoja
watoto wa masikini na watoto wa tajiri
huwezi kuwatofautisha pindi wachezapo.
• Hawapendi makuu,MFANO UNAWEZA
KUMWAMBIA SHUKA KWENYE KOCHI NA
UKAE CHINI,NAYE HUKAA MUDA ULE ULE.
• Watoto wadogo HUPENDANA wana
upendo mzuri
• Hawashikilii mambo Mfano WANAWEZA
KUGOMBANA WAO KWA WAO NA GAFLA
UKIPITA MUDA MDOGO TU,WANAKUWA
PAMOJA WAKICHEZA hawashikilii hasira.
• Watoto wadogo wana DHAMILI
SAFI,ISIYOKUWA NA HATIA Mfano MTOTO
WA KIKE ANAWEZA KULALA MPAKA
ASUBUHI NA MTOTO WA KIUME BILA
KUFANYA CHOCHOTE TENA HATA
WAKILALA UCHI,AU HATA KAMA
WATAKWENDA KUOGA PAMOJA WAO NI
SAWA TU maana dhamila zao zi safi mbele
za Mungu. N.K
Sasa mtu asipo GEUKA na kuwa na TABIA
kama hizo za watoto wadogo KAMWE
HAWEZI KUINGIA KATIKA UFALME WA
MBINGUNI.
JE WEWE UME UKOKA NA KUONGOKA ?
-Au umeokoka bila kuongoka ?
-Au umengoka bila kuokoka ?
Watu wa DINI wao wanaweza kuwa
wameongoka,na kufuata amri na sheria za
dini zao lakini HAWAJAOKOKA na hawana
mpango wowote wa kuokoka na
wakijidanganya kuwa DINI zao kwamba
zitawapeleka mbinguni,au kwa kuongoka
kwao,
Mimi leo ninakutangazia Kuongoka kwa
DINI yako KAMWE HAKUKUINGIZI
MBINGUNI BILA KUOKOKA
KWANZA,ukishaokoka ndipo mchakato wa
kuongoka unafuata.
Na yule aliyeokoka ,asipoongoka KAMWE
HAWEZI KUINGIA KATIKA UFALME WA
MBINGUNI
Mfano ;
Tazama wanafunzi wa Yesu ,wao walokuwa
wameshaokoka,Lakini bado Yesu Kristo
anawaambia na kuwasisitiza WAONGOKE.
( Mathayo 18 : 1-3 )
Haleluyaaa..
Kumbuka ;
Mchakoto wa kwenda mbinguni kwanza
UOKOKE kisha ufanye kuukulia wokovu
yaani KUONGOKA
Ukishaokoka ndipo unafanya mazoezi ya
kugeuka kabisa kwa mwenendo wako wa
kwanza na hapo ikiwa utafanya hiyo
utafanana na mtoto mdogo.
NI OMBI LANGU KWAKO,
KWAMBA KUONGOKA /KUBADILI
MWENENDO WAKO WEWE WENYEWE
HAUWEZI BILA MSAADA WA YESU KRISTO
ULLIYEMPOKEA,
SASA UMSIHI SANA MUNGU AKUPE
UJASIRI NA UWEZO KUACHA KILA JAMBO
BAYA NAYE ATAKUGEUZA UWE MALI
YAKE .
UBARIKIWE.

SHERIA YA DHAMBI

Mch. Josephat Gwajima (SNP)

UTANGULIZI:

Warumi 8:1-2 “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.” Katika huu mstari wa pili tunaona sheria tatu ambazo Biblia inazitaja, kwanza sheria ya uzima, sheria ya dhambi na sheria ya mauti. Dunia hii inaongozwa na sheria (principles) na ndio maana kuna katika ulimwengu wa kawaida kuna sheria mbalimbali. Mfano sheria ya mvutano (gravitation force) na ndio maana ukichukua jiwe ukalirusha juu litakwenda lakini baada ya muda litarudi chini tena. Na kimsingi huwezi kubishana na sheria hiyo, na ukitaka kuibishia jaribu kwenda gorofani ujirushe lazima utaanguka chini sio kwasababu huna upako bali ni kwasababu ya sheria ya mvutano inayovuta vitu kuja chini.

DUNIA YA KAWAIDA NA SHERIA ZILIZOPO: Kwa kawaida sheria huwa hazibadiliki, kwa mfano sheria inayosema unavyopanda kwenda juu baridi linaongezeka, hii sheria haibadiliki na ndio maana katika mlima kuna baridi zaidi kwasababu ya sheria ambazo zipo. Na vilevile sheria tulizoziona katika Biblia (warumi 8:2) ni bayana yaani hazitanguki. Na kwa maana hiyo hata nchi ili iwe na amani ni lazima ziwepo sheria na kanuni. Na ili watu wafuate sheria wamewekwa polisi, mahakama na magereza kwaajili ya kuhakikisha zile sheria zinafuatwa.

Unapofanya kosa lolote, unaingia kwenye matatizo kwasababu ya sheria iliyopo, kwa namna hiyo polisi watakukamata na kukupeleka mahakamani unapogundulika una makosa unafungwa, hii yote ni kwasababu ya sheria iliyopo.

MAISHA YA KIROHO NA SHERIA YA UZIMA, DHAMBI NA MAUTI: Kama tulivyoona sheria za nchi zinazosimamia maisha ya wananchi ndivyo sheria hizi za rohoni zinavyotenda kazi. Kimsingi unapovunja sheria ile sheria inakushusha chini bila ya wewe kujua. Na ndio maana biblia inasema “kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele” Kuna tofauti kati ya mshahara na zawadi, kwasababu unapotenda kazi ni lazima upokee mshahara wake, upende usipende na ulieusilie.

Kimsingi, wewe unaweza ukawa unatenda vitu na hakuna anayekuona, unaweza ukawa umeokoka lakini unatenda mambo mabaya au dhambi katika ulimwengu wa siri. Siku utakayopokea mshahara kila mtu atajua isipokuwa hatojua umepokea hilo kutoka katika kazi dhambi gani uliyotenda. Unaweza kumuona mtu alikuwa wa Mungu lakini akafa ghaflaghafla watu wakasikitika na kumbe umepewa mshahara wa matendo yake ya sirini. Maisha yako ya sirini ni muhimu sana.

SHERIA YA DHAMBI:
Warumi 6:23: “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.”

Ezekieli 18:4: “Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa.”

Nini maana ya maneno haya?; hapo mwanzo sheria alikuwa mbinguni, akifikia kipindi akafanya yaliyomaovu na kuasi hivyo akafukuzwa mbinguni. Na alipotupwa duniani akaanzisha utawala wake katika kila mtaa wa dunia hii ili kutenda kazi kila mahali. Haya majeshi ya pepo wabaya yapo kwaajili ya kuwapa watu mishahara ya matendo mabaya wanayoyatenda.

Kwasababu shetani alikuwa mbinguni, anaifahamu biblia anajua kanuni za Mungu, hivyo, unavyotenda lililoovu shatani anajua kuwa umekosea na amekaa tayari kugawa mshahara. Kumbe mshahara huu hautoki kwa Mungu bali shetani ndiye alipaye. (Yohana 10:10) yaani shetani hatendi kazi isipokuwa kuharibu, kuchinja na kuharibu. Unapotenda uovu kwa siri, mashetani hukaa mahali ili kugawa mshahara wa uovu ile. Na kwa muda ambao mashtaka yapo na hayajakanushwa kwa kutubu, mtu huyo atajikuta anafia dhambini. Kwa namna hiyo watu wengi wanaishi kwenye magonjwa na matatizo yanayotokana na maisha yao ya sirini ambayo hakuna anayejua.

Kiukweli hakuna dhambi ndogo wala kubwa, hivyo dhambi iliyondogo sana yaweza kumpeleka mtu Jehanamu. Dhambi ambazo watu huzidharau na kuziita ndogo ndizo zipelekazo watu Jehanamu bila hata ya wao kujua. Jifunze kutubu kila unapojikuta unamkosea Mungu.

Ni muhimu kutafuta mahali ulipouacha upendo wako wa kwanza, uhurudie na ukatubu. Mungu ni mwenye rehema atakusamehe kabisa na hatoyakumbuka makosa yako tena. Tengeneza maisha yako ya rohoni.