Saturday, March 9, 2013

FAHAMU NINI MAANA YA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA







Nini maana ya kusifu na kuabudu
KUSIFU NA KUABUDU ni maneno
tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu
MAANA --- nikuelezea wasifu au
wajihi za kitu au mtu. Sasa
tunaposema tunamsifu Mungu
inamaanisha ni KWA KUMUINUA
JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA
SAUTI,KUFANYIA SWANGWE,
KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA
UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4
Neno hili kusifu kwa kiebrania
lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa
kuongeza vionjo na mbwembwe
zaidi. Mfano neno haleluya
unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee)
Tehila ni kuwa kama kichaa
unaposifu au kuabudu kwa utukufu
wa Bwana. (Nilidhani labda hapa
ndipo waswahili walipopata neno
taahila).
Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu
(you just surrender yourself to the
Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za
Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni
yeye peke yake anayestahili heshima
na utukufu. Huwezi kumpigia saluti
mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia
ya kumwabudu Mungu katika roho
na kweli ndipo tunapomwona kama
alivyo na utukufu wake
2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina
maana ya kuabudu, kusujudia,
kuinama kwa kuonesha
unyenyekevu, kuonesha heshima
kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno
la Agano la Kale proskuneo
halikadhalika lina maana ya kubusu
mkono, au kupiga magoti na kugusa
ardhi kwa paji la uso kwa
unyenyekevu mkuu. Maneno
mengine mawili ya kuabudu yana
maana ya kutumika, kufanya ibada
Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.
Waache Watu Wangu Waondoke, Ili
Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu
alilolirudia mara kwa mara lilipelekea
Farao kuwaruhusu watu wa Mungu
kutoka Misri. Tangu wakati huo,
Mungu, Mungu mwenye wivu,
amekuwa akipambana na watu wake
akiwazuilia kuabudu miungu mingine
na sanamu, na badala yake
wamwabudu Mungu aliye hai na wa
kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na
kumfurahia daima. Mungu
anawatafuta watu wa kumwabudu,
na kufanya ibada ndiyo wito wetu
wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja,
tena ipo, ambapo wale waabuduo
halisi, watamwabudu Baba katika
roho na kweli. Watu wanaoabudu
namna hii, ndio Baba anawatafuta.
Msitari wa 24 unasema Mungu ni
Roho na wote wanaomwabudu
imewapasa kumwabudu katika roho
na kweli.). Ibada ya kweli ni pale
tunapomruhusu Roho Mtakatifu
atuongoze kutoka katika roho zetu
au mioyo yetu kuabudu katika roho
na katika kweli na sio tumaini letu
ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.
Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni
la kipekee na linamhusu Mungu
(utatu mtakatifu) ambao peke yao
wanastahili. Lucifer, aliyekuwa
mhusika mkuu wa ibada huko
mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa
ajili yake, maana yake aabudiwe
yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo
lililopelekea kuanguka kwake (Isaya
14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani
alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe
falme zote za dunia lakini Bwana
alikataa Mt4:8-10.
Kwa hiyo kuabudu ni ibada na
tunaposema ibada sio zile taratibu
za kibinadamu tulizojipangia katika
ibada zetu za siku za leo, ibada za
leo tumeweka mambo mengi sana
na yanatumia muda mwingi sana
kuliko ile maana hasa ambayo
mungu aliikusudia katika agano la
kale utana ibada zilikuwa zinafaywa
kwa mambo makuu 2 neno la
Mungu, na Kuabudu.
Kuabudu ni sehemu ya maisha
wanadamu tumeumbiwa kuabudu,
watuwezi kuishi bila kuabudu hapa
haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza
kuwa unaabudu Mungu wa kweli au
miungu kama ambavyo ukisoma bilia
utaona kuna miungu mingi inatajwa
mfano Baali, Dagon ink na hata leo
iko miungu mingi ambayo wanadamu
wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni
mmoja tu. Na katika biblia tunaona
kuaudu kwa mara ya kwanza
kulikofanywa na Ibrahimu kutoka
katika kitabu cha mwanzo 12: 8
Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa
kumwabudu Mungu kila wakati.
Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu
kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm
29:2 Tunapomwabudu mungu naye
Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah
3:17 Rom 12:1-2
Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano
wa mungu ulivyo ndani yako,
haijarishi unaabudu wapi uwe peke
yako au mko wengi kama unaabudu
kwa kutokumaanisha au kumaanisha
itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu
anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo
wako kwa Mungu wako.
KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA
KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26
zinaonyesha ambavyo kwa kutumia
kusifu tu Mungu alishuka na kufanya
lile lililokuwa hitaji lao.
Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa
unasifu na kuabudu humfukuza adui
mbali kutokana na ukiwa kwenye
ibada Mungu hushuka maana yeye
anasema anakaa katikati ya sifa
hivyo palipo na Mungu shetani
hawezi kuwepo lazima akae
mbali.akimbie mbali kabisa maana
kunakuwepo na uwepo wa bwana
wa Majeshi.
Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu
Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa
Zaburi ya 100 inatuelekeza namna
ya kuanza, lakini zaidi ya yote
tunapaswa kuishi maisha ya ibada
bila kukoma. Kwa kila tunapopumua,
kwa kila wazo, kwa neno na tendo,
tunapaswa kumwabudu Mungu wetu
mzuri tunayemtumikia milele na
milele Zab 145:1,2
mwa 12:6- Siku zilipita na watu
wakafanyia ibada kwenye Hekalu na
kwenye masinagogi; lakini siku hizi
miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor
6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada
zinatakiwa zifanyike kila wakati na si
mara moja kwa wiki kama wengine
wanavyo dhani.
Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu
walivyotumia mioyo yao, mawazo
yao, mikono yao, viganja vyao, miguu
yao, na midomo yao katika uimbaji.
Walipaza sauti zao kwa furaha na
kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki
na kushukuru.
Maneno kama halal na haleluya
kutoka katika Zaburi yana maana ya
kusifu, kumwinua na
kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah
lina maana ya kunyoosha mikono
hewani, na neno barak lina maana ya
kupiga magoti katika ibada ya
kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu
katika kumhudumia Mungu na
mwanadamu ni ibada pia (Rum
12:1). Watu pia humwabudu Mungu
katika sanaa zao, katika uandishi
wao, katika michezo ya kuigiza,
katika muziki, katika usanifu wa
majengo, na hata katika utoaji wa
fedha zao kwa ajili ya Injili.
Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na
kuabudu ni kuimba tu hapana kuna
njia nyingi za kusifu au kuabudu,
unaweza kutumia sanaa nyingine
kumwabudu mungu au watu
wengine wakamwabudu Mungu mf
maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji,
upambaji au unakshi wa vitu,
kujenga .nk
Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu
yanapaswa kujawa na zaburi,
nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo
zinaweza kuongozwa na Roho katika
lugha mpya anazotupatia Yeye.
Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa
haina tofauti sana na burudani za
kikristo kama kwenye kumbi za
starehe. Watu huwa wanaangalia tu,
lakini je, wanaabudu? Uwepo wa
Mungu na Roho wake katika ibada
zetu utawafanya watu wasioamini
kuanguka chini na kuabudu (Kol
3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe
5:19) (Mdo 2:4).
Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka
za kusifu. Daudi alicheza mbele za
Bwana kwa nguvu zake zote, na
akakataa kumtolea Mungu kafara
ambayo isingemgharimu cho chote
(2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi
wa Mashariki walitoa zawadi za
gharama kubwa walipokuja
kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na
mwanamke mmoja alimpaka Yesu
kwa mafuta ya gharama kubwa,
akamwosha miguu yake kwa
machozi yake, na kuifuta kwa nywele
zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada
yoyote inaambatana na kutoa tena
vitu vyetu vya thamani.
Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi
alivyo na kwa matendo yake; lakini
Mungu mwenyewe anawatafuta na
anawataka wafanya ibada, na si
mradi ibada tu. Kusifu kwaweza
kufanywa hadharani, lakini ibada
mara zote ni jambo la ndani ya
moyo. Kusifu mara zote kunaweza
kuonekana au kusikika, lakini
kuabudu yaweza kuwa ya
kimyakimya na iliyofichika. Kusifu
kunaonekana, kuna kutumia nguvu,
kuna misisimko na furaha; lakini
ibada mara zote ni heshima na hofu
katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi
Mungu anavyo hitaji na kutamani
kuabudiwa na yeye pekee yake
ndiyo anayestahili kuabudiwa.
Kusifu na kuabudu kwa siku za
leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa
mafundisho katika kusifu na kuabudu
na ndiyo maana ya kuanda somo hili
ili tupanuane mawazo. Watu wengi
wa leo wanadhani kusifu ni kuimba
kwa nyimbo zenye midundo ya
harakaharaka(zouk&sebene) na
ukipunguza spidi ndo kuabudu.
Hasha tunaposema kusifu inatokana
na maneno yaliyopon kwenye
wimbo husika kweli ni ya kusifu,
kama ni maneno ya kusifu tunasema
ni wimbo wa sifa haijarishi speed
inayotumika na hali kadhalika
nyimbo za kuabudu. Watu katika
kipengele hiki huwa wanachakanya
nyimbo utakuta wakati wa kusifu
anaimba wimbo wa kutia moyo au
wa maombi, kinachotakiwa ni kujua
kuwa kila jambo lina wakati wake
ziiko nyimbo za mazishi, kufariji,
kutia moyo, za maombi, za kusifu ,
na za kuabudu nk sasa usichanganye
kwenye kusifu wewe unaimba
parapanda italia au tuonane
paradiso, hizo sio za sifa sasa najua
wewe utafanya zoezi la nyimbo
unazozijua ili kufahamu zina ujumbe
gani na ziko katika kundi lipi kati ya
hayo niliyokufundisha hapo juu.
Baadhi ya maandiko yanayo
onyesha aina za kusifu na
kuabudu kwa:
1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)
2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)
3. Kuinama au kupiga magoti (Zab
95:6)
4. Kupiga makofi (Zab 7:1)
5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam
6:14)
6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)
7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law
23:40)
8. Kutembea (2Nya 20:21-22)
9. Shangwe (Zab 95:1)
10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law
9:23-24)
11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1,
32:11)
12. Ukimya (Mhu 3:7)
13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab
42:4)
14. Kulia/ kutoa machozi katika roho
mtakatifu
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza
ufalme wake na haki yake na hayo
mengine mtazidishiwa.

No comments:

Post a Comment