Tuesday, February 5, 2013

MAOMBI YANAYOZAA MATUNDA

Na-
MCHUNGAJI: FRANK ANDREW (RP)

UTANGULIZI:

Mungu anatuhitaji tuombe, tunatakiwa
tuombe sio tu kwasababu tunauhitaji
bali kwasababu Mungu anahitaji tuombe.
Tatizo la watu wengi wanashindwa
kupokea majibu ya maombi
wanayoomba na wengine wameshindwa
hata kuomba.wengine wamejikuta
wakikata tama bila kujua kuwa wao ndio
wanakosea katika kupeleka haja zao kwa
Mungu na katika kupokea. Hapa
tutajifunza sababu na jinsi ya kuomba ili
kupokea kutoka kwa BWANA.

SABABU NNE: KWANINI
TUNAMUOMBA MUNGU:

1. Kujinyenyekesha mbele za Mungu.
2. Kuonyesha kuwa yeye ni Mungu
wetu.
3. kuonyesha kuwa vyote viko mikononi
mwake
4. Tunampa heshima kama baba
mwenye familia ya watoto watakatifu.

MAOMBI YANAHUSISHA VITU
VIKUBWA VITATU:

1. Mhusika AU muombaji mwenyewe:-
huyu ndiye muombaji na mwanzilishi wa
maombi.
2. Maombi yenyewe:- haya ni mahitaji
au ujumbe ambao unapelekwa kwa
unaye muomba.
3. Unayemuomba:- unayemuomba ni
nani kwako na mna uhusiano gani naye.
Kwa kujua umuhimu wa kuomba,
wanafunzi wa Yesu walimwomba Yesu;
awafundishe jinsi kuomba na hapo Yesu
aliwapa fomula ya kuitumia ili kuomba.
Hii ndiyo inayoitwa sala ya BWANA,
kimsingi hii ni kanuni ya kuomba
aliyoifundisha Yesu na si maombi
yenyewe kama wengi wanavyodhani,

KANUNI hii ni sawa na kanuni yengine za
kufanya jambo fulani. Mfano kuna
kanuni za kupika au kanuni za kuimba.
Tatizo la watu wengi ni kwamba
wanatumia hii kanuni kama ndio
maombi yenyewe. Kwa mfano Yesu
aliposema “Baba yetu uliye mbinguni…”
alimaanisha kuwa unapokuwa unaanza
kuomba ni lazima ujue unamuomba
baba aliye mbinguni na si magomeni. Hii
ni kanuni jinsi ya kuomba na haitaji moja
kwa moja haja yako, bali ukiitumia kama
kanuni inakuletea majibu:=

Yakobo 5: 15-16 “kuomba kwake
mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa
bidii”, Biblia inaposema kuomba kwake
mwenye haki: anamaanisha kuwa yeye
anayeanzisha maombi ni lazima awe ni
mwenye haki yaani msafi. Kiukweli kuna
wakati mwingine Mungu hutenda
kwasababu ya neema yake lakini
kimsingi ili maombi yako yafae inabidi
uwe mwenye haki. Hivyo kabla ya
kuingia kwenye maombi unatakiwa
ujitakase kwanza ili Mungu akikutazama
aone uko safi. Ni muhimu kutengeneza
uhusiano mzuri na Mungu, tengeneza
haki kwanza kabla ya kuingia kwenye
maombi. Yaani kama hujaokoka uokoke
kwanza, na kama umeokoka lakini hauko
sawa na Mungu, unatakiwa utengeneze
maisha yako kwanza. Katika mstari wa
15* Biblia inasema “ungameni dhambi
zenu ninyi kwa ninyi” ikiimaanisha kuwa
kabla ya kuingia kwenye maombi
unatakiwa ujisafishe na ujitakase
kwanza.
Baada ya kujitakasa kinachofuata ni
kupeleka ujumbe wenyewe kwa Mungu.
Watu wengi kwasababu hukosea kuomba
wamedhania kuwa Mungu huwa hajibu
maombi; lakini Biblia inasema Mungu
anajibu maombi. Biblia inasema, Zaburi
2:8 “uniombe nami nitakupa mataifa
kuwa urithi wako...” na katika Mathayo
7:7 “Ombeni nayi mtapewa…” kumbe
unapoomba lazima Mungu akujibu kama
ukiomba sawasawa na mapenzi yake. Ni
muhimu kabla ya kupeleka hoja yako
uamini kwanza kuwa Mungu yupo
sawasawa na Waebrania 11:6 “...lazima
aamini kuwa Mungu yupo”. Haya
maandiko tutatumia katika kuangalia
jinsi ya kuomba na wapi watu wengi
wanapokosea wakiwa katika kuomba…

KANUNI ZA KUPOKEA KUTOKA KWA
MUNGU:

Watu wengi wanajua kuomba lakini kati
yao wengi hawajajua namna ya kupokea.
Kwasababu kuna namna ya kuomba na
namna ya kupokea. Watu wengine
wanajua kuomba lakini hawajui jinsi ya
kupokea haja zao. Haifaidii kitu kujua
kuomba na huku ukiwa hujui jinsi ya
kupokea. Kuna mambo kadhaa ambayo
unatakiwa uyatilie maanani unapokuwa
unaomba kama ifuatavyo:-

1. Tengeneza uhusiano wako na
Mungu:-
Maandiko yanasema “haja zenu na
zijulikane mbele za Mungu” pamoja na
kuwa Mungu anajua haja zetu lakini bado
anahitaji sisi tumuombe. Hii ni sawa na
kuomba kwa jirani wakati baba yako
mzazi yupo; utajisikiaje mtoto wako
anapokuwa na shida alafu akuombi
wewe baba yake, alafu yeye
anajitengenezea sanamu na kuiomba.
Utakavyojisikia ni sawa kabisa na Mungu
anavyojisikia kwetu ndio maana Mungu
anasema kuwa anaona wivu (kutoka
20:4) . Mungu anataka tumuombe yeye
ili kujenga uhusiano na yeye. Ukiomba
au kuiabudu sanamu unamfanya Mungu
awe na wivu.

2. Unaongea nini ukiwa katika
maombi yako:-
Maombi unayoongea kwenye maombi ni
ya muhimu sana kwenye kupokea haja
zako kutoka kwa BWANA. Ttuangalie
kwa habari ya Hana; 1Samweli1:1-24; Elikana alikuwa na wake wawili
Penina na Hana, kama lilivyojina lake
Hana hakuwa na watoto kwasababu
tumbo lake lilikuwa limefungwa. Hana
hapo kwanza alikuwa anaenda na
malalamiko na kulia. Watu wengi
hupeleka malalamiko kwa BWANA,
badala ya kupeleka hoja kwa Mungu.
Hata siku moja Mungu atendi jambo bila
kusudi, na ndio maana tumbo la Hana
lilikuwa limefungwa kwa muda wote ule.
Emu tuangalie mambo kadhaa
yaliyokuwa yakimzuia Hana.
>Sababu ya kuomba:-
1Samweli 1:1-24 Hana alikuwa
anamuomba Mungu ampe mtoto ili
amkumeshe penina, na ndio sababu
inayowafanya wengi washindwe kupokea
kwa BWANA kwasababu hawana sababu
ya Kibiblia inayowafanya Mungu awape
mahitaji yao. Mfano mtu anamwomba
Mungu mke ili amfulie nguo au
amechoka kuishi mwenyewe. Hiyo si
sababu; Mungu anahitaji hoja yenye
nguvu ili upokee mwambie jukumu lako
la kutimiza kwenye maisha yako na
nafasi ya mke katika kumtumikia Mungu;
hapo lazima akutendee.

>Peleka haja ya moyo wako:-

Mungu haitaji hali yako ikoje sasa bali
anahitaji kujua unataka nini. Picha ya
tatizo lako unatakiwa uwe nayo wewe
lakini mbele za Mungu unatakiwa
upeleka haja ya moyo wako na si
malalamiko. Kwa wakati ule Hana
alikuwa anapeleka hali yake ilivyo na
penina na si uhitaji wake kwa BWANA.
Unakuta mtu anamuomba Mungu gari ili
awaonyeshe wengine, huyo hawezi pata
kwasababu si sawa na mapenzi ya
Mungu.

>Mwangalie Mungu na si jambo
unalohitaji:

Ibarahimu alipompokea Isaka
ilimradhimu Mungu kumjaribu ili ajue
upendo wake upo kwa Isaka au kwa
Mungu. Watu wengi wanamuomba
Mungu jambo lakini wakilipokea ndilo
linalofanyika mzigo mkubwa wa
kutokumtumikia Mungu, mfano mtu
anaomba mume akipokea tu; baada ya
siku chache haji kanisani anasema eti
anamuhudumia mumewe. Kwasababu
hii hata Hana akupata mtoto mpaka
alipobadilisha maombi na kumuomba
Mungu mtoto, kwa kumuahidi BWANA
kumtoa mtoto huyo awe mtumishi
wake.

3. Imani na Bidii:
Watu wengi wanafikiri bidii ni kutumia
nguvu tu katika maombi, bali bidii ni ule
mzigo; ni muhimu unapokuwa unaomba
uwe na mzigo wa kuombea. Ili uzae
matunda katika maombi ni lazima uwe
sawa na mama mjauzito aliye katika
kuzaa; lazima uwe na uchungu yaani
umaanishe. Vivyohivyo kupokea kutoka
kwa BWANA Unatakiwa umaanishe na
lazima uamini pia kuwa ni wakati wako
wa kupokea kutoka kwa BWANA.
Unapoomba unatakiwa moyo na akili
yako iwe kwenye kile unachohitaji. Kuna
watu wanabidili maombi kila kukicha kwa
kuhisi kuwa Mungu awasikii lakini bidii ni
kubaki kwenye jambo hilo hadi uone
amani moyoni kuwa BWANA
ameshatenda na hili jambo ndilo ambalo
Eliya alilifanya alipokuwa anaomba mvua
kunyesha tena. Eliya alikuwa
mwanadamu wa namna moja na sisi
alikuwa na Bidii katika maombi.

JAMBO LA KUFANYA:

Baada ya kujua mambo haya ni muhimu
kubadili mtazamo wako na jinsi
unavyoomba. Mungu anajibu maombi
kama ukiomba sawasawa na neon lake.
Kwanza uwe na picha ya kile ambacho
unataka BWANA akutendee, uombe na
imani na bidii. Hapo lazima Mungu
akutendee kwasababu hakuna baba
ambaye mwanaye atamwomba mkate
akampa jiwe au samaki akampa nyoka.
Badili mtazamo wako katika maombi
yako ili uwe mpokeaji wa maombi yako
ni si mwombaji asiyepokea chochote!!!

-FRANK ANDREW-
Resident Pastor G.C.T.C

Sunday, February 3, 2013

WAKATI UFAAO KUANDAA SILAHA YAKO.

Na; CONRAD CONWELL
Silaha hutengenezwa wakati wa
amani,wakati wa vita ndipo
hutumika....."WAKRISTO wengi wakati wa
amani hawaombi,ila mambo yakigeuka
kidogo hufunga na kuomba,Wakati wa
kuzama si wakati wa kujifunza kuogelea bali
ulipaswa kujifunza kabla,fanya maazimio ya
kumtafuta MUNGU wako siku za amani na
simama kwenye zamu yako
kikamilifu,Mtafute Mungu wako kwa Bidii...
Mithali 8:17
Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Andaa na uvae silaha
sasa,
Luka 21:34-36.
Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima. Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.
"BWANA MUNGU AWABARIKI NA KUWAPA NGUVU ILI KUWEZA KUANDAA SILAHA "

MATUKIO YA KICHAWI (sehemu ya pili)

UTANGULIZI:
Watu wengi wanajiuliza kwanini
tunazungumzia uchawi mara nyingi, hii ni
kwasababu shetani hutumia wachawi
katika kutenda kazi duniani; na ndio
maana katika Biblia kuna maandiko
mengi yanayotaja uchawi na wachawi
kama ifuatavyo:- Hesabu 23:23 24:1;
1Wafalme 9:22; 2Wafalme 17:17;
Isaya 47:9,12; Mika 1:12; Nahumu
3:4; Matendo ya Mitume 8:9; 18:11;
Wagalatia 5:20; 3:1; Ufu 9:21. Ni kweli
tumepewa mambo yote na Mungu kama
vile afya na mafanikio lakini shetani
kupitia wachawi amekuwa akizuia, hivyo
tunatakiwa kushughulika nao katika
ulimwengu wa roho.. Katika sehemu ya
kwanza ya somo hili tuliona kwa habari
ya Ayubu ambapo shetani alipata ruhusa
ya kugusa maisha yake. Shetani
hakumtokea Ayubu kwa namna ambayo
angemfahamu kuwa ni shetani, lakini
alimjia kwa njia ya matukio, kumbe
waweza kuwa unapitia kwenye hali
mbaya kumbe ni matukio
yanayosababishwa na wachawi.
Wakristo walio wengi wanapambana na
shetani bila kujua nguvu za adui wanae
pamaba nae. Nchi ya Japani ilipokuwa
haijui kuwa Marekani wana bomu la
nyuklia; waliwachokoza wakidhania kuwa
watashinda, Lakini matokeo yake
walishindwa kwasababu walikuwa
hawajui nguvu ya wanayeshindana naye.
Mara nyingi watu wengi hupambana na
shetani bila kujua nguvu zake na
matokeo yake wengi huishia kushindwa.
Huwezi kupambana na adui usiyemjua,
vivyohivyo ili uweze kumshinda shetani
ni lazima uanze kwa kutafuta maarifa
kuhusu yeye.
MAFURIKO YA KICHAWI:
Ufunuo 12:13-16 Yule Joka alikuwa
shetani, Biblia inasema Yule joka akatoa
maji kama mto; kwa kawaida
ingeonekana kama mafuriko ya maji
dhidi ya yule mwanamke. Kumbe kuna
matukio yanaweza kutokea kwenye
maisha yako au kwenye nchi, na kumbe
yamesababishwa na wachawi. Si kila
moto au mafuriko ni ya kiasili, mengi
huwa yanasababishwa na shetani ili
kuua watu ili awashushe kuzimu. Kuna
matukio yanatokea unadhania kuwa ni
ya kawaida kumbe yameletwa na
wachawi ili kuangamiza watu. Ni
muhimu kujifunza kuyaangalia matukio
kwa jicho la rohoni.
BIASHARA ZA KICHAWI:
Ezekieli 28:16, 18. “kwa wingi wa
uchuuzi wako; watu walikujaza
udhalimu” shetani mfanya biashara naye
hutenda kazi pamoja na wachawi na
waganga wa kienyeji. Kwa njia hii
shetani anafunga maisha ya watu, na
ndio maana kuna watu wanafanya
biashara za kichawi, Yaani
wanamwendea shetani halafu
wanamuomba aiwezeshe biashara yao
kwa kumpa shetani ama damu au
kafara. Wachawi wanapokuwa wanatoa
kafara, huwa wanakuwa wanafanya
biashara na shetani. Ufunuo 18:1-
mstari 5” “wafanya biashara wa nchi
wamepata mali kwasababu ya kiburi
chake” mstari 11” “nao wafanya
biashara wa nchi walia na kuomboleza
maana hapana mtu anunuaye bidhaa zao
tena” mstari 13 ” biashara ya roho na
miili ya wanadamu. Kumbe biashara
nyingi unazoona watu wanafanya
duniani, ni biashara za kichawi. Yaani
mtu anafanya biashara lakini ndani yake
kuna uvuvio wa kishetani, Nahumu 3 : 4 .
Ndio maana biashara za watu wengi
hazifanikiwi wakati huohuo watu
wanaomtegemea shetani wanafanikiwa
kwa haraka ni kwasababu wameuza roho
zao kwa shetani.
Matendo ya Mitume 16:16-17; 19:24
“aliyewapatia bwana zake faida nyingi”
biashara hizi zipo kabisa, na ndio maana
unaweza kufanya biashara lakini
wenzako wanauza zaidi kuliko wewe
hata kama wote mnauza bidhaa ileile,
kumbe wenzako wamenuiza ili wao
wauze na wewe usiuze. Ni vizuri kuanza
kufanyabiashara na BWANA, yaani kabla
ya kuanza biashara ni muhimu kufanya
maombi kwanza ili kuiweka biashara
yako katika ulinzi wa Mungu. Unapotaka
kuanza biashara fanya na BWANA.
MAGONJWA YA KISHETANI:
Kuna watu ni wagonjwa sasa kwasababu
ya wachawi. Magonjwa mengi sana
husababishwa na wachawi. Unaweza
kuwa unasumbuliwa na magonjwa
yasiyopona kwasababu ya chanzo chake
ni cha rohoni. Na ndio maana
unapooumwa hata kama utaenda
hospitali unatakiwa usiache maombi
kwasababu shetani anaweza kusababisha
magonjwa, hata Ayubu aliumwa majipu
mabaya ambayo kimsingi yalisababishwa
na shetani.
BIBLIA NA MATUKIO YA KICHAWI:
Mathayo 9:32 “tazama walimletea mtu
bubu mwenye pepo, na yule pepo
alipotolewa alinena” huyu ni mtu
ambaye watu walipomuangalia
walimuona ni bubu. Cha ajabu Yesu
alipomuona hakushughulika na ububu
bali alishughilika na pepo kuonyesha
kwamba ule ububu ulisababishwa na
pepo. Kuna mambo mengi ambayo
yanasababishwa na shetani, hivyo
unatakiwa kuyashughulikia.
Mathayo 13:10-15 “alikuwa na pepo wa
udhaifu kwa muda wa miaka kumi na
nane…” 15” “na huyu mwanamke aliye
uzao wa Ibrahimu ambaye shetani
shetani amemfunga” watu walishamzoea
kumwona kuwa ni mama mwenye
kibiyongo yaani hawezi kujinyoosha
kabisa lakini Yesu alipomtoa pepo Yule
mama alipona.
Wachawi wapo na watu wengi
wanalogwa, Kumbukumbu la Torati
18:11 ; watu wanalogwa na wanalogeka,
matatizo ya watu wengi yanasababishwa
na shetani kupitia matukio ya kichawi.
Marko 9:17 ; kuna magonjwa ambayo
yanakuja kwenye maisha ya mtu
kwasababu ya kulogwa. Katika utendaji
kazi wa shetani anaweza akaingia ndani
ya mtu na kumfunga, lakini pia shetani
anaweza kumkandamiza mtu akiwa nje
ya mwili na ndio maana kwa watu
waliokoka lakini hawapigani vita ya
rohoni wanaweza kujikuta
wanakandamizwa na shetani akiwa nje
yao. 1Wathesalonike 2:18 , Paulo
hakuwa amepagawa na pepo lakini
shetani alimzuia. Zekaria 3:1 . Shetani
anaweza kukuzuia kutokea nje, yaani
unahitaji kwenda nje ya nchi lakini
shetani anakuzuia kupitia mtoa pasi ya
kusafiria. Matendo ya Mitume 13:6
hata wachawi hupambana pia ili
kukuzuia, ni muhimu kuishi maisha huku
ukijua kunakushindana rohoni.
JINSI YA KUSHINDA DHIDI YA
MATUKIO YA KICHAWI
Mpokee Yesu kwanza; huwezi
kushindana na shetani kama hujaokoka,
ni muhimu umpokee Yesu kwanza ili
akuwezeshe kupigana katika vita dhidi ya
shetani. Jifunze kuomba mwenyewe;
baada ya kuokoka kuna amani ya
mwanzo unayoipata ile isikufanye
ukasahau kuwa tupo vitani, kama
tulivyoona hapo juu wanaoshindana
nawe wanaweza kuwa ndani yako au nje
yako. Katika hali hiyo unachotakiwa
kufanya ni kujifunza kuomba mwenyewe
kwasababu hata ukitegemea kuombewa
kila siku, kuna muda utakuwa
mwenyewe, na hapo unatakiwa
usimame mwenyewe. Mtu uliyeokoka
unatakiwa uhame kwenye ule wokovu
wa kuombewa uhamie kwenye wokovu
wa maarifa na kupambana kwa kutumia
Jina la Yesu Kristo.